Nimezaliwa Afrika, naipenda Afrika na naitakia mema Afrika. Leo nimeamua kuperuzi kuhusu bara langu na haya ndiyo niliyokumbana nayo.
Afrika ni sehemu
inayovutia sana na ni bara lenye utofauti mkubwa duniani. Ni nyumbani kwa watu
wa aina tofauti, wanyama, hali ya hewa na maeneo ya kuvutia. Ni bara
linalojulikana kwa mavazi yake mazuri ya rangi na historia ya kazi nzuri ya
sanaa. Afrika ni mahali ambapo binadamu wa kwanza alionekana dunani.
Watu wa Afrika
Graca Machelni ni mwanamke pekee duniani aliyewahi kuwa mke wa Rais
wa nchi mbili tofauti Afrika Kusini na Msumbiji
Bara la Afrika
ni la pili duniani kwa idadi kubwa ya watu. Watu bilioni moja na ushee.
Watu wa Afrika wanaongea zaidi ya lugha elfu moja, baadhi ya makadirio yanaweka hii namba karibu na elfu mbili.
Dini kubwa Afrika ni Uislamu ikifuatiwa na Ukristo.
Watu wa Afrika wana idadi ya wastani wa asilimia 14.72 ya idadi ya watu duniani (Taarifa: Umoja wa Mataifa 2009)
Watu wa Afrika wanaongea zaidi ya lugha elfu moja, baadhi ya makadirio yanaweka hii namba karibu na elfu mbili.
Dini kubwa Afrika ni Uislamu ikifuatiwa na Ukristo.
Watu wa Afrika wana idadi ya wastani wa asilimia 14.72 ya idadi ya watu duniani (Taarifa: Umoja wa Mataifa 2009)
Kuna watu wengi wanaongea kifaransa Afrika kuliko nchini
Ufaransa.
Mabaki ya binadamu mkongwe yaligundulika Ethiopia, yana takribani umri wa miaka 200,000.
Watu wa San kutoka Afrika Kusini mpaka leo bado
wanatumia zana zilizokutwa mapangoni kutoke miaka 44,000 iliyopita.
Wanariadha wengi wa mbio za kasi duniani wanatoka
kwenye kabila moja la Kalenjins kutoka Kenya.
Rais wa kwanza wa Zimbabwe alikuwa anaitwa Rais Banana.
Mfumo wa ardhi
Afrika
Mto mrefu duniani
upo barani Afrika, Nile wenye urefu wa maili 4,132.
Afrika ina jagwa
kubwa duniani, Sahara ambalo lina ukubwa takribani sawa na Marekani.
Victoria falls
ni maporomoko makubwa ya maji barani Afrika; lina urefu wa 355ft na upana wa
maili moja.
Mlima
Kilimanyaro (Tanzania) ni mlima mrefu barani Afrika na wapili kwa urefu duniani,
19,300ft. Mlima huu ni mrefu sana kana kwamba barafu inapatikana kileleni kwake
japokua mlima upo karibu na ikweta.
Madagaska ndicho
kisiwa kikubwa Afrika na kisiwa cha nne kwa ukubwa duniani. Kisiwa kipo Bahari
ya Hindi kwenye pwani ya Afrika Mashariki.
Bara
Afrika ni bara la pili kwa ukubwa duniani, lenye
eneo la mraba takribani maili 117M. Kwa namna nyingine Afrika ni kubwa kuliko China, Marekani, Mexiko, India na sehemu kubwa ya bara la ulaya likijumliswa.
Bara la ulaya na Afrika zinatenganishwa na Kilometa
14.3 tu za bahari na kuna maungeza ya kutengeneza daraja refu duniani.
Afrika ni bara lenye joto kuliko yote duniani.
Sudani ndiyo nchi kubwa Afrika, eneo la mraba wa
maili 968.000.
Kairo ndio mji mkubwa Afrika.
Afrika imekatwa na ikweta.
Wanyama
Mnyama wa ardhini mkubwa duniani, ni tembo wa
Afrika.
Mnyama mrefu duniani,ni Twiga, Anaishi Afrika.
Mnyama wa ardhini mwenye kasi duniani ni Duma.
Anaishi Afrika
Afrika ni nyumbani kwa reptile mkubwa duniani,
Mamba wa Nile.
Gorila anayeweza kukutwa kwenye misitu ya bara la
Afrika, ndiye Nyani mkubwa duniani.